Esther alilifikia gari la Boss France huku akiangua kilio kikubwa na kizito sana wakati huo wafanyakazi wenzake na watu wangine
waliofika katika eneo lile walikuwa wakifanya juhudi za kumuwahisha Boss
France hospital kwa ajili ya kuokoa maisha yake Naye Esther ambaye ndiye
aliyekuwa Sekretari wa Boss France aliwataka wampandishe Boss France katika
gari lake kwani kwake ilikuwa ni ngumu kuweza kuendelea kusubiria gari la
wagonjwa lifike katika eneo lile huku akiona hali ya Boss wake kuwa mbaya
zaidi.
Na hatimaye watu waliokuwepo katika
eneo la tukio walimpandisha Boss France katika gari ya Esther huku Esther naye
akiwa ni msaada tosha katika hilo kwani naye alikuwa amembeba Boss wake na
kumpandisha ndani ya gari huku akiendelea kububujikwa na machozi. Alimuomba
mmoja wa wafanyakazi wenzake aliyekuwepo katika eneo lile kumtaka kumsindikiza
kuelekea Hospital ingawa umati mkubwa
uliokuwa eneo lile ulitamani kufanya hivyo kama sehemu ya kumkarimu Boss France
ambayd alikuwa ni kipenzi cha wengi. na mara moja bila ya kutaka kupoteza muda
Esther aligeuza gari lake na kuliondoa kwa mwendo wa haraka huku shauku yake
kubwa ni kuhakikisha anafanya kila uwezekano wa kuokoa maisha ya Boss wake.
Basi kulingana na mwendo aliokuwa nao Esther
haikuwachukua muda sana kuikaribia Hospital Looh! Kwa kadri walivyozidi
kusogea walianza kuyaana maandishi ya AGA-KHANI HOSPITAL kwa ukaribu
zaidi. Kwa bahati mbaya hiyo ndiyo
hospital iliyokuwa imemlaza Vicky mmoja wa wafanyakazi wa Hyatt Regency
The Kilimanjaro Hotel aliyekuwa akihusika na kitengo cha uhasibu.
Esther aliingiza gari hadi ndani ya geti na mara moja wahudumu wa huduma ya
kwanza waliweza kufika kwa ajili ya kumpokea Boss France na kuanza kumpatia
huduma za kitabibu. “Ooooh! My God sikuweza kutaraji jambo kama hili” Esther
alinena huku akishusha pumzi kwa uzito wa tukio lile.
Wakati huo Esther pamoja na yule mmoja
ya wafanyakazi aliyeambatana naye walikuwa wakiendelea kufuatilia kwa ukaribu
juu ya huduma alizokuwa akipatiwa Boss France.
Esther alikuwa mwenye kuhaha na mwenye
hofu kubwa juu ya Boss wake mpaka kufikia hatua ya kutamani kumuuliza kila
daktari na nesi aliyekuwa akikatiza mbele ya macho yake juu ya hali ya Boss
France. Esther na mwenzie waliendelea kuketi kwenye moja ya sofa za wageni
waliokuwa wakiwasindikiza wagonjwa wao pale hospital. Kwa mbali kuna daktari
mmoja aliyekuwa akitembea kuja katika eneo alilokuwa ameketi Esther na mwenzie,
na baada ya hatua chache aliweza kuwasili mahala pale “Habari za Asubuhi,
naitwa Dr.Adamu ni Dkt mkuu msaidizi wa AGA-KHANI
HOSPITAL” aliyasema
hayo Dr. Adam naye Esther alidakia “Esther hapa sekretari mkuu wa Hyatt
Regency The Kilimanjaro Hotel”
aaaah! Kumbe ndiyo wewe, aliitikia Dr.Adam kwa mshangao mkubwa na akiwa
na imani kwamba Esther na mfanyakazi mwenzie walikuja pale kwa ajili ya kumuona
Vicky aliyeletwa na Boss France na kulazwa hapo usiku wa kuamkia siku hiyo pasipo
kufahamu kilichomkuta Boss France.
Dr.Adamu aliendelea kuwasemesha akina
Esther “Nadhani bila shaka mtakuwa mmeshafuata taratibu zote basi mnaweza
kwenda kumuona mgonjwa wenu na amelazwa wodi namba 5 V.I.P” maneno hayo
ya Dr. Adamu yaliwashtusha akina Esther kwani wodi namba tano ilikuwa ikihusika
kuwalaza wagonjwa wa jinsia ya kike. “Mmmmh, Kwani Dr.Adam mbona mgonjwa wetu kama vile ameingizwa
upande mwengine na bado yumo kwenye matibabu” aliyasema hayo Esther
huku akimtolea macho Dr.Adamu kwa mshangao mkubwa, Alaaah! Naye Dr.Adam alishtuka na
kuanza kufikiri huenda akawa ni mtu mwingine muhimu ndani ya Hyatt Regence
The Kilimanjaro Hotel.
Kwani uwepo na sekratari ulimpa maswali
mengi zaidi. Aliendelea kufikiri kwa muda huku akijiuliza kwamba mtu huyo
huenda angekuwa ni nani maana masaa machache nyuma alikuwa na Boss France pale
Hospital hivyo hakutaka kuamini kama angekuwa ndiye lakini ghafla alikumbuka
lisaa limoja nyuma mpaka kufikia muda huo namba ya Boss France haikuwa
ikipatikana akataka kulithibitisha hilo kwa kuendelea kuipigia namba ya Boss
France. “Asante kwa kutumia mtandao wa Vodacom namba unayoipigia
haipatikani kwa sasa tafadhali jaribu tena badae” na hayo ndiyo majibu
aliyoambulia Dr. Adamu kutoka kwenye simu yake. Looh....! Weee.
Mapigo ya moyo yalimwenda mbio Dr.Adamu
na alipomtazama Esther kwa wakati huo alimuona amejiinamia huku akiendelea
kutokwa na machozi. Dr. Adamu aligeuka kwa Haraka dizaini ya Mwanajeshi
aliyekuwa akikwepa risasi na kukimbilia katika chumba cha wagonjwa wa dharura
na alipofika alitizama kulia na kushoto kwa haraka haraka Daaah!.. Alifanikiwa
kumuona Boss France aliyekuwa amejeruhika katika eneo lake la usu pamoja na
mguu wa kulia, alijisikia huzuni sana na
hapo kumbukumbu ya usiku wote wa jana ikamjia juu ya namna ambavyo Boss France
alikuwa akipambana kuhakikisha Vicky anarejea katika hali yake. Alitoka nje
bila ya kumsemesha mhudumu yeyote aliyekuwa ndani ya eneo lile nao walibaki kumshangaa
Dr.Adamu pasipo kupata majibu sahihi juu ya jambo lile
Dr.Adamu alielekea katika eneo
alilokuwa amekaa Esther na mwenzie na ghafla Esther alisimama haraka na
kumsogelea Dr.Adamu na kutaka kujua juu ya hali ya Boss France. “Kuna
nini kwani?, Kipi kinachoendelea Dr.Adamu” Aliuliza Esther aliyeonekana
kuwa na wimbi kubwa la moyo wa majonzi. Dr. Adamu alieendelea kukaa kimya huku
akimtazama Esther machoni. Kitendo hicho kisichokuwa na majibu kiliendelea
kuongeza jeraha ndani ya moyo wa Esther na kumfanya aendelee kulia kwa uchungu.
Kuna nini jamani?
Ilisikika sauti nzito iliyotekea upande wa kushoto wa eneo walilokuwa watatu
hao Sauti hiyo nzito ambayo ilikuwa ya kwanza kutambulika na Dr. Adamu haikuwa
ya mwingine tofauti na Dr. Justine ambaye ndiye alikuwa ni Daktari mkuu wa pale
AGA-KHANI HOSPITAL. Wote walishtuka na kutizama sauti ile ilipokuwa inatokea “Ahaah!
Karibu Boss” alikuwa ni Dr. Adamu aliyeyasema hayo huku akipeleka mkono
wake wa kulia mbele kutaka kumsalimia Dr. Justine. “Asante sana... mbona
mko katika hali hii” aliendelea kuuliza Dr. Justine huku akimtizama Dr.
Adamu. Baada ya kimya kidogo Dr. Justine alimtaka Dr. Adamu aweze kuambatana
naye kuelekea katika ofisi yake ili kuweza kufahamu zaidi juu ya tukio lile.
Wakati huo naye Esther aliyekuwa katika hali ya majonzi na wimbi la kusongwa na
mawazo kichwani mwake alianza kufikiria juu ya kile kilichotokea asubuhi na
mapema wakati Boss France alipompigia simu na kumuuliza juu ya kikao cha siku
hiyo. “Nakumbuka aliniuliza juu ya kikao lakini nadhani hakutaka kuishia
hapo kwani kuna jambo jingine alilotaka kunijuza wakati nilipokata simu yake” alijiuliza
Esther katika fikra zake na kuhisi huenda palikuwa na kitu za ziada asubuhi ile
alipopigiwa simu na Boss wake.
Ndani ya ofisi ya Dr. Justine yaliendelea
mahojiano baina yake na Dr. Adamu juu ya yale yote yaliyokuwa yametokea naye
Dr. Adamu alisimulia matukio yote kuanzia usiku aliompokea na kumlaza Vicky
aliyekuwa chini ya uangalizi wake kwa maagizo ya Boss France. Aseee! Dr.
Justine alihuzunika sana kwani Boss France alikuwa ni mmoja wa marafiki zake
wakubwa aliyesoma naye chuo kimoja huku kila mmoja akisomea fani tofauti na pia
alikuwa ni m,bia mwenzake waliokuwa wanashea hisa katika kampuni ya Vodacom.
Na hapo hakutaka kupoteza muda kwani
alihitaji kuelekea moja kwa moja katika chumba alichokuwemo Boss France. Alitoka
ndani ya ofisi yake huku akioneka mwenye haraka ya kutaka kuwahi kumuona rafiki
yake Boss France. Alifika ndani ya chumba alichokuwemo Boss France na wakati
huo naye Esther alisimama na kukimbilia katika eneo la chumba hicho. Kwa bahati
mbaya Esther alizuiliwa kuingia ndani ya chumba hicho na kitendo kile
kiliendelea kuivuruga sana akili yake kiasi cha kutamani kuuvunja mlango ule
ili aingie ndani walau kumwona Boss wake. Dr. Justine alimtizama Boss France
ambaye kwa wakati huo alianza kurejesha fahamu zake huku akiita “Vicky...
Vicky... Vicky...” Maneno hayo aliyokuwa yakimtoka Boss France
kwa sauti kubwa yaliweza kumshtua Esther aliyekuwa amesimama pale mlangoni
kisha akajiziba mdomo wake uliokuwa ukitaka kutoa sauti ya mshtuko ule na
kuanza kupata picha halisi ya tukio lile la asubuhi kuhusu simu ya Boss wake.
Papo
hapo bila ya kufikiri sana Esther alianza kutoka mbio kukimbilia katika wodi
namba 5 ili kujua na kuthibitisha ni
mgonjwa gani aliyekuwemo mule V.I.P lakini wakati akianza kuyafanya hayo kichwa
chake kiligeuzwa na sauti iliyokuwa ikimuita kwa msisitizo mkubwa, “Boss, Boss, Boss.
Sekretari” alikuwa ni yule mfanyakazi aliyekuja naye pale hospital
kumleta Boss France aliuliza Esther “Khaa! Mbona hivyo umenishtua sana wewe
kwani kuna nini?” “kuna namba ngeni imepiga hapa lakini inaonekana kama vile
niya taasisi fulani” alizungumza yule mfanyakazi huku akiikabidhi simu
kwa Esther ambaye alipokea namba ile moja kwa moja bila ya kufikiri juu ya
jambo lolote. “Hello! Unaongea na Inspekta Nyawenga hapa, nipo katika
eneo la tukio la ajali pamoja na timu yangu nzima. hivyo tunakuhitaji haraka
sana.” Na ndicho alichokutana nacho Esther punde tu baada ya kupokea
simu ile. Loooh! Mapigo ya moyo wa Esther yalimwenda kasi kiasi
cha moyo wake kutaka kumchomoka na mbaya zaidi hapakuwa na nafasi ya yeye
kuhoji juu ya suala lile zaidi ya kufuata maelekezo. Mwili wake ulikufa ganzi
na kudhoofu ghafla, mithili ya mti
uliopigwa na radi na asijue ni nini cha kufanya kwa wakati huo.
***Mwisho***
Je
ni nini kitakachoendelea na kipi atakachokifanya Esther baada ya kuanza kupata
majibu ya kile alichokuwa anakihisi juu ya simu ya asubuhi ya Boss france na
baada ya kupata simu ya dharura kutoka kwa inspecta nyawenga.?
Endelea
kufuatilia miendelezo ya tamthiliya pendwa ya pesa za shemeji. Sehemu ya nane 8
jumamosi ijayo.
MWANDISHI SEBASTIN SEBA
MAWASILIANO: 0746445197
EMAIL;masabaseba123@gmail.com

0 Comments