Looh! Almanusura Vicky
agongeshe kichwa chake ukutani lakini zilikuwa ni Juhudi za Boss France
aliyeruka kama mwewe
aliyeona
kifaranga cha kuku kikiteatea na kukinyakua mara moja. Kwa mikono yake Boss
France Vicky alipata usalama usiokuwa na malipo. Ilibidi wamlaze na kuendelea kumpatia
matibabu chini ya uangalizi wa Dr. Adam. Kiza cha usiku wa manane kilikuwa
kimeshatanda na ngurumo za upepo kutoka bahari ya Hindi zilikuwa zikisikika,
Minazi nayo ilikuwa ikiyumba kuelekea kulia na kushoto, JiJi la Dar-es-salaam lilikuwa tuli huku
liking'arishwa na Mianga ya taa zilizoonekana kila upande.
Basi
Kutokana na uchovu aliokuwa nao Boss France alianza kusinzia pale kitandani
naye Dr. Adam hakuwa na neno baada ya kumhudumia Vicky alitoka na kuelekea
katika ofisi yake. Majira yalizidi kusonga huku kimya cha kutosha nacho kikiwa
kimetawala kwani hapakuwa na hata mmoja wa kumsemesha mwingine kwa wakati huo huku
kila mmoja akiwa katika wimbi zito la usingizi. Mara ghafla Boss France alishtushwa
na Sauti ya Vicky iliyosikika kuhitaji msaada wake “Boss
France nisaidie” “Boss France hauwezi ondoka” “Boss France nisaidie” sauti hiyo iliendelea kusikika mara kadhaa ingawa
ilikuwa ya ladha yake lakini ilimtia uwoga Boss France na kumfanya amtolee
macho Vicky, mapigo ya moyo yakamwenda kasi huku jasho jembamba likianza
kumtiririka. Lakini Baada ya muda mfupi Boss France aligundua kuwa ile ilikuwa
ni ndoto ambayo Vicky alikuwa akiiota huku akiweweseka , ikamlazimu Boss France
aheme kwa kushusha pumzi na mapigo ya moyo yakaanza kupungua taratibu.
Alisimama
na kuangaza kulia na kushoto na hakuweza kubaini chochote kile cha tofauti
zaidi ya kuona mandhari iliyokuwemo mule ndani. Haikuchukua masaa mengi
mwangaza ulianza kuonekana kwa nje na kiza kilianza kutokomea wakati huo Vicky
alikuwa bado katika hali ya usingizi mzito,
Naye Boss France alifikiri zaidi juu ya shughuli za kiofisi. Alimsogelea
Vicky kisha akamshika katika mkono wake wa kulia na kupeleka mdomo wake ulioachilia
busu zito huku akijisemea moyoni mwake kwamba “Usijali Mamaa lazima
nihakikishe unakuw salama siku zote” zilikuwa ni hisia nzito na zenye
kusisimua kutoka kwa Boss France ambazo zingemfanya Vicky ajione yupo katika Dunia
ya tofauti lakini haikuweza kuwa hivyo kwani Vicky kwa wakati huo, hakuweza
kutambua chochote kilichofanywa na Boss France kutokana na hali ya kuwepo
katika wimbi zito la usingizi.
Boss
France aligeuka na kuanza kuujongelea mlango kisha akaufungua na kotoka nje
huku macho yake yakimtazama Vicky aliyeoshesha uso wa tabasamu na wenye kuvutia
ingawa bado alikuwa amelala. Alielekea moja kwa moja katika ofisi ya Dr. Adamu akabisha
hodi kisha akaingia ndani, Alimsalimu kama ilivyoada na tamaduni zetu sisi Watanzania
naye Dr.Adamu hakusita kuichangamkia salamu ile ya Boss France. Baada ya salamu
Boss France alizamisha mkono katika mfuko wake wa nyuma na kuchomoa wallet yake
kisha akiifungua na kutoa kiasi kingi cha noti za elfu kumi akampatia Dr.Adamu
na kumtaka amhakikishie juu ya usalama wa Vicky naye Dr. Adam alimhakikishia
hilo Boss France. Walipokwisha kukubaliana waliagana kisha Boss France
akatizama saa yake ya mkononi na kuona kwamba ilikuwa imekwisha kutimia majira
ya saa kumi na mbili kasoro Asubuhi. Laaah! “Sijui leo itakuwaje kuhusu
kikao sidhani kama nitawahi kweli” alijisemea Boss France huku
akitembea haraka kuelekea nje alipopaki gari lake na alipofika kama kawaida
yake hakusita kuanza kulikagua kwa macho na baada ya kujiridhisha akaingia
ndani ya gari na kuliwasha huku akiwa na hesabu za kuelekea kwanza nyumbani
kwake Oyster bay alianza safari
na kabla hata ya kufika mbali alipokea simu yake ya mkononi iliyosikika kwa
sauti ya mtu aliyetaka kufahamu alipolazwa Vicky.
Ilikuwa
ni vigumu sana kwa Boss France kuweza kutoa majibu ya moja kwa moja kwa sababu
alihofu sana juu ya usalama wa Vicky na alifikiri mbali zaidi kwa sababu
hakuweza kuitambua sauti ile ilikuwa niya nani. “Samahani naongea na nani?”
alihoji Boss France “naitwa Calvin mmoja ya wale waliokuwa
wameambatana na Vicky kuja kule HAVOC NIGHT SPOT CLUB”…. “Ohooh!...”
aliitikia Boss France kwa mshangao. Hakuweza kuendelea kujadili sana
kwa ajili ya hilo kwani alikuwa na safari ya kuwahi kuelekea nyumbani kwake
Oyster bay kwa kufikiri hilo alimuelekeza ni wapi alipolazwa Vicky lakini kabla
ya kuendelea na safari yake alikumbuka juu ya Erick mmoja wa mabamnsa wa HAVOC
NIGHT SPOT CLUB aliyeambatana naye siku ya usiku wa jana wakati wakimpeleka
Vicky Hospital. Ila Kwa bahati mbaya hakuweza kuwa na mawasiliano yake kwa
wakati huo hivyo ikambidi asijali sana kwa kuhisi kwamba lazima Erick atakuwa
salama na hasa akizingatia uzoefu wa kazi yake. Aliendelea na safari ya kuwahi
nyumbani kwake ingawa palikuwa na umbali wa kiasi chake lakini hakujali
hilo, njiani alikuwa ni mtu mwenye wingi
wa mawazo hasa akiwaza zaidi kuhusu Vicky pamoja na kikao cha siku hiyo. Na
mbaya zaidi Vicky naye alikuwa ni mmoja ya wakuu wa vitengo mbalimbali ndani ya
HYATT REGENCY HOTEL hivyo Boss France aliwaza ni majibu gani hasa angeyatoa
mbele ya wajumbe wengine wa kikao kile juu ya kile kilichomkuta Vicky. La
hasha!.. Ulikuwa ni mtihani mzito.
Safari
ya kwenda nyumbani kwake Oyster bay ilianza kusuasua akafikiri kwamba ni bora
zaidi aelekee moja kwa moja eneo lake la ofisi kwani angeweza kupata huduma
zote ingawa ilikuwa ni mapema mno tofauti na mda wake uliozoeleka wa kuingia
kazini. Lakini zuri zaidi palikuwa na
duka la nguo aina ya suti ambapo kwake yeye isingeweza kuwa changamoto kuweza
kuzipata kulingana na uwezo aliokuwa nao ingeweza kuwa rahisi kwake kukubaliana
na mawazo yake hasa akizingatia na ugumu wa foleni ya magari yaliyokuwa mbele
yake kwa muda huo.
Aligeuza gari na kuelekea kazini kwake, wakati
akiwa njiani alichukua simu yake na Kumpigia Sekretari wake Esther lakini simu yake iliita kwa muda mrefu
bila ya majibu hivyo hakuwa na budi kupiga kwa mara nyingine na baada ya mda
mfupi ilisikika sauti ya Mrembo Esther aliyekuwa akizungumza kwa mapozi ya
usingizi La hasha!.. Ilikuwa ni sauti nyororo nayakuvutia kiasi kwamba asingetamani
kukata simu hata baada ya kueleza jambo lake. “Hello Boss France Kwema
kweli mbona leo simu ya mapema sana…..? Alizungumza kwa kuvuta maneno “Yes
ahaah… no yeap ni kwema kiasi” “Yeap yeap ni kwema” Boss
France aliendelea kuzungumza huku akiwa na kigugumizi kikali lakini Esther
aligundua kwamba kuna jambo la tofauti kwa hali ile aliyoibaini kutoka kwa Boss
wake. “Kuhusu kikao maandalizi
yako vipi?” aliuliza Boss France “Ndiyo Boss hakuna kilichokaa
vibaya mambo yote yako sawa” lilikuwa ni jibu la Esther baada ya swali
la Boss wake.
Boss France alitamani kumjuza Esther juu ya
kile kilichomkuta Vicky lakini mdomo wake ulikuwa mzito dizaini ya mtu aliyewekewa
gunzi mdomoni hivyo hakaona isingeweza kuwa sahihi kwa wakati huo kumjuza
Esther juu ya tukio lile. Basi Esther
aliamua kukata simu baada ya kuona kimya cha muda naye Boss France alisikika
akiita “Eeesther wewe Eee…..” Aliishia kusema hivyo. Looh! Kuna
namna ambavyo Boss France alianza kuchanganyikiwa na msongo wa mawazo, aligongagonga mikono yake kwenye ustelingi wa
gari huku akionyesha hali mithili ya mtu mwenye mgogoro na nafsi yake. Lami ilikohoa
vumbi kwa namna ambavyo Boss France alikuwa akiendesha lake na haikumchukua mda
alikuwa amekaribia kufika katika eneo la HYATT REGENCY HOTEL lakini siku
hiyo ilikuwa ni siku ya kutimia kwa msemo kwamba “Asiye na bahati habahatiki
kamwe” kwani kutokana na msongo wa mawazo aliyokuwa nao Boss France ulimpelekea
kufanya vitu visivyo sahihi. Aliendeshe gari kwa mwendo wa kasi mno na ghaflaa…
alipokuwa akikata kona kuingia katika geti la HYATT REGENCY HOTEL huku akijaribu
kushika breki ya gari kwa haraka alijikuta akilivaa geti na gari kujigonga na
mkito wa sauti ile ulisikika kwa sehemu kubwa ya eneo hilo na kuwashtua wengi.
Na hapo Boss France alipoteza Fahamu na kishindwa kuelewa kilichokuwa kikiendelea kwa wakati huo. Kelele kubwa ya “Uwiiiiiiii jaman Boss France… Boss France…” iliyosikika kwa nguvu iliendelea kuwashtua wengi na kukimbilia eneo la tukio na ilikuwa niya mmoja wa wafanyakazi wa usafi aliyebahatika kushuhudia tukio lile lililomkuta Boss France ili kutaka msaada wa haraka. Watu wengi sana walijazana katika eneo lile huku kila mmoja akiwa na taharuki ya tukio lile. Haikuchukua mda kwa Esther aliyekuwa akielekea kazini kufika katika eneo lile kwani naye aliamua kuwahi kazini siku hiyo na ni baada ya kuhisi hapakuwa na utimamu kwa Boss France. Alishuka mara moja katika gari lake na kutupa pochi yake kutokana na mshtuko alioupata huku akilikimbilia gari la Boss France na kulia kwa sauti ya huzuni “Mungu wangu jamani Boss France Mamaa Boss wangu jamani…….”
Je, ni nini kitakachotokea Baada ya tukio lile
lililomkuta Boss Fance ambaye alimwacha Vicky Hospital na kuahidi kumhudumia
kwa kila hali?

1 Comments
Kazi nzuri sana big up
ReplyDelete