Facebook

PESA ZA SHEMEJI SEHEMU YA KUMI (10)

 

A story by Sebastian Masabha

0758-162527

Boss France aliendelea kumkumbatia vicky, wakati huo Esther aliyekuwa akiendelea kudondosha machozi yake nyuma ya Boss France alikodoa macho kwa nguvu zote ili kujaribu kumfahamu mwanamke aliyekuwa amekumbatiana na Boss France. Dkt Justine na jopo lake la madaktari na manesi nao hawakuwa na chakufanya zaidi ya kuendelea kuwatizama Vicky pamoja na Boss France wakiwa wanabadilishana joto la miili yao. Esther hakuwa tayari kuendelea kukubaliana na hali ile aliyokuwa akiishuhudia mbele ya macho yake kwani alisogea karibu na kuwavaa akina Boss France pamoja na Vicky.

La hasha!.. naye Dkt Justine alijikuta akiropoka “Hapana, hapana Esther usifanye hivyo”  lakini Esther hakujali juu ya kauli ya Dkt Justine kwani wimbi zito la wivu wa kihisia juu ya Boss France lilishamvaa na kujitoa fahamu kwa lolote lile mahala pale. Dkt Justine aliendelea kufoka “Wewe Esther ina maana haujui kwamba mimi.......” kisha akasita kuendelea kuzungumza na kuanza kujigonga, gonga kichwani mwake Looh!.. ama kweli ilikuwa ni vita ya waziwazi ya kihisia iliyokuwa ikimtesa kila mmoja kiasi cha kusema “unachokikataa wewe mwenzio kina mnyima usingizi” kwani yalikuwa ni mapigo ya mpigiko yaliyoupiga moyo wa kila mmoja.

Haikuwa rahisi kwa Esther kuelewa wala kumsikiliza yeyote yule zaidi ya Boss France kwa wakati ule kwani ndiye aliyekuwa tazamio lake pasipo ya Boss France kuligundua hilo. Esther alishtushwa kiasi cha kwamba ilimbidi harudi hatua mbili nyuma baada ya kutambua yakuwa mwanamke aliyekuwa amekumbatiana na Boss France alikuwa ni Vicky. Alifyonza kwa nguvu na kwa kejeli “Mfyuuuu....Mshenzi mkosa akili, kumbe ni wewe mwanamke mpenda hanasa” alitoa maneno hayo ya kejeli huku akimtizama Vicky kwa kumpandisha na kumshusha mara tatu tatu kwa macho yake ya asali.

Vicky hakujali kuhusiana na kejeli zilizokuwa zikimtoka Esther katika kinywa chake kwani naye alimtizama Esther kwa dharau na kisha akaupeleka mdomo wake na kumpiga kisi zito Boss France aliyekuwa haelewi upande wa kulia ni upi na wala upande wa kushoto ni upi kwa wakati huo.

Baada ya hatamu fupi wakiwa bado pale Hospitali Boss France alipigiwa simu na mtu aliyeshindwa kumtambua kwa wakati huo. Simu hiyo ilipigwa na mtu aliyetanguliza salamu za pole kwa Boss France kutokana na madhila yaliyomkuta na kumfanya kuwepo pale AGA KHAN HOSPITAL kwa muda wa siku kadhaa. Mazungumzo baina ya Boss France pamoja na mtu huyo yaliwafanya akina Esther, Vicky,  Dkt Justine na wengine wote waliokuwa katika eneo hilo wakae kimya na kuendelea kusubiri juu ya kile kilichokuwa kinaendelea. “Habari Boss! Pole na madhila yaliyokusibu na kupelea kushindwa kuendelea na shughuli za kulijenga taifa kwa siku kadhaa” mtu huyo alizungumza na Boss France pasipo kuweka utambulisho wake lakini alionekana kuwa ni mtu aliyemfahamu vema Boss France. “Ahsante sana ndugu lakini napata wasi kujua naongea na nani” alihoji Boss France kutaka kufahamu alikuwa akizungumza na mtu gani. “Naitwa PRINCE ALPHONCE ni mkaguzi mkuu wa makampuni na mashirika ya umma na yasiyo ya umma hapa nchini,  nimefanya mazungumzo na wewe ili kupata kibali cha kutembelea Hoteli yako yenye hadhi ya NYOTA tano kikazi zaidi.” Alijitambulisha mtu huyo na kupata ukaribisho mzuri kutoka  kwa Boss France ambapo waliafikiana kwamba ugeni huo utapaswa kuwasili siku mbili mbeleni.

Haikupita hata dakika Boss France akapigiwa simu tena kwa njia ya Whatsapp video call na mmoja wa wafanyakazi wake Waooooh... Ilikuwa ni suprize kwake kwani alichokiona katika kioo cha simu yake lilikuwa ni jopo la wafanyakazi wenzake kutoka katika idara tofautitofauti wakiwa na shauku ya kutaka kufahamu hali aliyokuwa nayo Boss wao kwa wakati huo.

Zilikuwa ni nyuso mbalimbali zilizoonyesha tabasamu murua kwa kufurahi kuona Boss wao akiendelea vema. “Hi.. Boss we miss you.. so much..” ilikuwa ni sauti ya mmoja wa wafanyakazi wake aitwaye Nice aliyeshindwa kuzuia hisia zake kwa kummiss Boss wao kwa siku kadhaa. Esther alimgeukia Dkt. Justine na kutaka kujua juu ya gharama za malipo ambazo kampuni ingepaswa kugharamia juu ya matibabu ya Boss France. Wakati akihoji hilo naye Boss France alidakia na kuchomekea neno. “Je vipi kuhusu Vicky? kwani hautambui yakwamba naye alilazwa hapa kwa siku kadhaa” Heeh!... Jambo hili lilionekana kuwa jipya kwa Esther ambaye hakuwahi kufahamu lolote lililomkuta Vicky na kupelekea kuwa pale Hospital. Esther akaanza kujiuliza na kujisemea katika moyo wake na fahamu zake “Alaah inawezekanaje ya kwamba Vicky alikuwa amelazwa hapa siku zote hizo pasipo ya mimi kuwa na taarifa”.

Kisha akatikisa kichwa na kuendelea kujihoji “Ahaah! Sasa nimehisi kitu nadhani ndo ile siku niliyopigiwa simu asubuhi na Boss France na badae akataka kuniambia juu ya jambo fulani alafu akasita ahaa! Nadhani ndivyo nimeshapata majibu” pamoja na hayo yote na kutokana wimbi la wivu wa kihisia lililokuwa likizidi kumpanda kichwani mwake akaona aendelea kujipa maswali na kukujibu ili kuiridhisha nafsi yake. “ Sasa kwanini Boss France akuniambia?,  kwanini anifiche? na wakati mtu alipata matatizo au alihisi nitamvurugia kwa Vicky? haaaah! Kumbe Boss France atakuwa anampenda sana Vicky. Je,  vipi watakuwa wameshafanya lolote lile lakini hapana maana Vicky alikuwa ni mgonjwa Huhuhuu.. Mimi sijui bhana ngoja niyaache” Baada ya Boss France kumhoji jambo Esther na kuona ukimya umetawala aliamua kumuita “Wewe Esther unawaza nini mbona kama akili yako haipo hapa? Akaongezea tena kwa mara nyingine Vipi kuhusiana na Vicky Je,  kampuni haimtambui? Esther alishtuka na kutoka katika lile wimbi la mawaza na akaona kwamba alichokuwa akikiwaza ni ujinga mtupu.

Kampuni itahusika Boss wangu ila kwa vielelezo maalumu vinavyoonyesha chanzo cha yeye kuwepo hapa maana kama kampuni hatukuwa na taarifa ya Vicky na wala wewe hukuwahi kunijuza chochote kuhusu kulazwa kwa Vicky hapa Hospital. Baada ya majibu hayo Boss France aliona kwamba hakuna haja ya yeye kuendelea kuitaka kampuni ihusike na gharama za matibabu ya Vicky kwani kuendelea kufanya hivyo kungesababisha Esther pamoja na wafanyakazi wenzake waweze kutambua siri nyingi katika yake yeye na Vicky. “Basi naona itakuwa ni prosesi sana hivyo mimi binafsi nitagharamika na gharama zote za matibabu za Vicky zilizosalia” alijiwahi Boss France kusema hivyo huku akiwa na lengo lake kichwani wa kutaka kuepusha mlolongo wa mambo yaliyojificha.

Baada ya Dakika kadhaa bili zote za matibabu ya Boss France pamoja na Vicky zililetwa na mmoja ya wafanyakazi waliokuwa wakihusika na kitengo cha uhasibu pale Hospitali kutokana na Amri ya Dkt. Justine. Alikuwa ni mdada aliyekabidhi bili zote mbili za matibabu kwenye mikono ya Boss France. Boss France hakuweza kusema chochote zaidi ya kutoa ghuno na kukaa kimya huku akimtizama yule Dada machoni mwake. Boss France alipaswa kulipa kiasi cha Milioni tatu kama sehemu ya gharama zilizotumika kumtibu Vicky. Wakati huo gharama za matibabu yake zikiwa ni Millioni nne na laki tisa kitu ambacho akikuweza kusumbua kichwa chake kwani kampuni ndo ilipaswa kugharamika juu ya matibabu yake.

Alichukua bili ile na kumpatia Esther huku mkononi mwake akiwa na bili ya matibabu ya vicky. Kwa wakati huo aliona ni ngumu kuondoka na kwenda kuchukua kiasi hicho cha pesa mahala alipo zihifadhi, ikambidi kumpigia simu mmoja wa marafiki zake wakubwa na Boss mwenzake aliyekuwa ni Meneja katika Hotel kubwa ya SERENA HOTEL ambayo nayo ipo katika orodha ya Hotel zenye hadhi ya NYOTA tano Jijini Dar-es-salaam. Boss huyo alifahamika kwa jina la Meneja Tinno maarufu kama sultani ambapo lilikuwa ni jina alilopachikiwa na wafanyakazi wenzake kutokana na mwonekano wake wa kufuga ndevu nyingi zilizokuwa zimejitapakaza hadi mashavuni mwake mithili ya mzee mkavu.

Boss Tinno kwa kutambua umuhimu wa rafiki yake mkubwa na ambaye wamekuwa wakishindana pakubwa katika kuzitangaza na kuziendeleza Hotel zao za NYOTA tano kama mameneja hakuwa na budi kumuagiza mmoja wa madereva wake kufikisha kiasi hicho cha pesa AGA KHAN Hospital. Esther aliandika hundi yenye malipo yaliyohitajika kulipia matibabu aliyofanyiwa Boss wake na wakati huo naye dereva wa meneja Tinno alikuwa akiwasili na kiasi cha pesa alichoagiziwa kumfikishia meneja Tinno.

 Walifanya malipo na kisha wakaagana na kumshukuru Dkt.Justine na timu yake kwa msaada na uangalizi wake mpaka kupona kwa wagonjwa wao.Baada ya zoezi hilo iliwabidi waanze  safari ya kuondoka kurejea majumbani mwao maana muda nao ulikuwa umeshasonga sana. Ilikuwa imeshatimu mishale ya saa kumi na mbili jioni. Esther aliafiki kwamba yeye angefanya jukumu la kumpeleka Boss France nyumbani kwake Oyster bay na kushauri kwamba angefanya pia jukumu la kumkodishia Vicky taks ambayo ingempeleka moja kwa moja hadi nyumbani kwake. Loooh.... Hapo Esther alikuwa ni kama amefanya kazi ya kuumwagia moto petrol kwani Vivky alimuangalia jicho baya utadhani alitaka kummeza mzima mzima.

 Lakini wakati hayo yakiendelea naye Dkt. Justine alikuja mkuku mkuku huku na bila ya kufikiria ya kwamba Esther alikuja na gari lake pale akaropoka “Mimi nitamdindikiza Esther mpaka nyumbani kwake na Boss France wewe utakwenda pamoja na Vicky” ikabidi wote wabaki kumtizama kwa kuona kama Dkt. Justine alikuwa amepagawa na kuhisi kwamba pengine yawezakuwa kuna kemikali zimemchanganya. Boss France alimshika Vicky na kumvuta pembeni ili kumnong'oneza jambo fulani naye mzee wa mikurupuko aliyechanganyikiwa kihisia na uwepo wa Esther akajaribu kumshika Esther mkono lakini loooh.. haikuwa kama ilivyokuwa kwa Boss France na Vicky kwani alikutanishwa na kofi la uso kutoka kwa Esther lililowashtua pia Vicky na Boss France na lililofanya miwani ya Dkt. Justine ianguke chini na kujishika uso huku akibakia kusema Lah! Lah! Lah!...

***MWISHO***

Endelea kufuatilia miendelezo ya  tamthiliya hii ili kupata mafunzi na burudani maridhawa

 

A story by Sebastian Masabha

0758-162527

Post a Comment

0 Comments