Facebook

PESA ZA SHEMEJI SEHEMU YA TISA (09)

 

Esther alishuka kwenye gari lake na kapanda ngazi mkuku mkuku kuelekea katika ofisi ya Dkt. Justine. Alifika mlangoni akagonga mlango lakini hakukuwa na ishara wala sauti yeyote aliyoweza kumkaribisha ndani, akaendelea kugonga mlango ule mpaka mara tatu na kimya nacho kikaendelea vilevile ikabidi afungue mlango na kupenyeza kichwa chake ndani ili kuona kama palikuwepo na mtu. Alishtuka kidogo baada ya kuona yakuwa hapakuwa na mtu ndani, ikambidi atoke na kwenda kwenye ofisi ya Dkt. Adamu na kisha akafanya kama alivyofanya kwenye ofisi ya Dkt. Justine lakini kwa bahati mbaya ofisi ya Dkt. Adamu ilikuwa imeshafungwa.

Punde tu, aligeuza shingo yake na kutizama kulia na kushoto bila ya kuweza kuwaona wahusika wake na hapo akarudisha mawazo nyuma kukumbuka kwamba alimwacha Grace pale Hospital kwa ajili ya kumpa taarifa juu ya Boss wake Boss France. Alichukua simu yake kutoka katika mkoba  na kisha akaipigia namba ya Grace lakini pia haikuwa bahati kwa muda huo kuweza kumpata Grace kupitia njia ya mawasiliano ya simu kwani simu yake haikuwa hewanikwa mda huo.

Lakini alibaki akijiuliza kwamba angeweza kumpata wapi, lakini kwa bahati nzuri wakati akiyawaza hayo kwa mbali aliweza kumuona Dr. Justine akirejea katika ofisi yake, naye hakutaka kupoteza muda ikabidi amfuate hukohuko.

Wakati akitembea kwa haraka haraka na kufika nje ya mlango wa ofisi ya Dkt. Justine kisha akauzuia mlango ambao ulikuwa ukifungwa na Dkt. Justine aliyekuwa akiingia ndani ya ofosi yake. Kefule!!!... Nini tena?,  Ahaah! Kumbe ni wewe karibu sana” alizungumuza Dkt. Justine, mithili ya mtu aliyejiuliza na kujijibu mwenyewe. Asante Dkt. Justine” aliitikia Esther ambaye alikuwa katika hali ya kutaka mambo yake yaweze kwenda kwa uharaka. Dkt. Vipi kuhusu hali ya mgonjwa wangu nahitaji kufahamu hilo” aliuliza Esther huku akimtizama  Dkt. Justine katika macho yake. Unapaswa kusubiri mgonjwa wako atakuwa sawa  tu” alijibu Dkt. Justine huku akionyesha hali ya kutokujali sana juu ya Esther. Maskini Esther alishusha pumzi kidogo kutokana na jibu la Dkt. Justine na kisha akaupeleka mkono katika blauzi yake na kulegeza kifungo kimoja cha juu huku akijipepea kwa tishu nyepesi.

Madoido na mitego ya Esther kwa Dkt. Justine haikuishia hapo kwani alianza kuyachezesha macho yake huku akidai kwamba palikuwa na Joto mule ndani licha ya Viyoyozi vyote vya ofisi ile vikiwa vimewakwisha kuwashwa.

Dkt. Justine alizidi kuhamaki na hakuamini juu ya kile kilichokuwa kikifanywa na Esther na hapo alipeleka mawazo na akili yake mbali zaidi kwa kuhisi kwamba siku hiyo ingeweza kuwa siku ya bahati ya mtende kana kwamba aliona ni kama amekwisha kuliokota Dodo chini ya mti wa mkwaju.

Esther aliendelea kumpagawisha na kumuhamisha zaidi Dkt. Justine kwa kitendo cha kulamba lamba midomo yake huku tabasamu lenye ladha ya mwani wa kipwani likimtoka. Eboooh! Dkt. Jastine alikuwa akimwangalia tu Esther huku akishindwa kuzungumza jambo lolote lile. Dkt. Justine alianza kushusha miwani yake na kuining'iniza chini ya macho yake  kisha akaanza kujichekesha chekesha dizaini ya mlevi aliyeona chupa ya balimi mbele ya macho yake,  wakati huo eneo la zipu ya suruali yake ilianza kupanda juu kama rocket iliyotaka kupaa angani. Na hapo Esther akaanza kuamini yakuwa mtego wake alianza kufanya kazi kikamilifu.

“Dkt. Justine” kukawa kimyaa... “Dkt. Justine” kukawa Kimyaaa tena,  Kisha Esther akaamua kugonga meza kwa nguvu na kuita tena kwa mara ya tatu “Hey! Wewe Dkt. Justine” naye Dkt. Justine akakurupuka dizaini ya mtu aliyeamshwa kutoka usingizini. “Naam naam ndiyo nipo Mwalimu” Kheee!!! Esther akamshangaa Dkt.Justine na kucheka kidogo kisha akaamuliza “Mwalimu wako katoka wapi tena hapa” naye Dkt.Justine hakuweza kujibu chochote hapo zaidi ya kuendelea kumtizama Esther.

Esther aliyeweza kuziteka fahamu za Dkt. Justine ndani ya sekunde chache mithili ya delila wa samsoni, Esther  alianza kujisifu na kujifurahia ndani ya moyo wake kwamba uzuri wake ndio ulioweza kuyafanya hayo yote. Esther alizidi kujikweza na kujisifu zaidi baada ya kupata mwanzo mzuri na mwepesi kwake kwa kufanikiwa kuutambua udhaaifu mkubwa wa Dkt.Justine ambao kwake ungekuwa ni fimbo na silaha ya kuweza kufanikisha matakwa yake.

“Dkt. Justine bila shaka ulinipigia simu na kuniuliza ya kuwa nilikuwa   wapi”  alihoji Esther naye Dkt. Justine akakimbilia kujibu kwa pupa bila ya kufikiria “Ndiyo nilitaka nikuone na hapo Dkt. Justine alijiingiza katika kesi isiyomuhusu mithili ya mbuzi aliyejitwika mafiga ya moto. Dkt. Justine alijikuta akilikubali swali la Esther na wakati hili suala lilikuwa nila Dkt. Adamu ambaye alimpigia simu Esther na kuitelekeza ofisi yake na kukimbilia Restaurant baada ya kuliona gari ya Esther likiwasili pale hospital.

Ilikuwa ni ishara tosha yakwamba Dkt.Justine alikuwa amekwisha jifia katika moyo ya Esther pasipo kujitambua, Dkt. Justine alijikuta akimpa Esther ushirikiano mkubwa juu ya Boss wake. Walitoka nje ya ofisi na kuelekea alipokuwa amelazwa Boss France Looh!!!.. Naye Esther alishindwa kuweza kujizuia kwa kukimbilia pale kitandani kwa Boss wake na kuanza kulia kwa machozi ya furaha baada ya kumuona Boss wake akianza kurejesha fahamu zake zilizokuwa zimetoweka siku kadhaa baada ya ile ajali.

 Dkt. Justune aliakuwa akimkata jicho Esther huku karoho kawivu kakianza kumtawala,  alijisikia vibaya kwa kuhisi kwamba mapenzi ya Esther yalikuwa yakijidhihirisha kwa Boss France. Wakati hayo yakiendelea kusawidi mara ghafla Boss France akaanza katamka maneno yaliyokuwa hayaeleweki zaidi sana kwa Esther. Boss France alianza kutamka maneno hayo huku akigaragara pale kitandani  “Huuuu... Huuuu...Nakuja,  nakuja  kukuchukua tuondoke naimani ushapona kwani nimekusubiri sana kwa muda mrefu” Looh!!! Na hapo Esther alijikuta akiyabadili machozi yake yaliyokuwa ya furaha na kuwa yenye uchungu mkubwa hata pia manesi waliokuwa pale nao walijikuta wakipata huzuni juu ya tukio hilo.

Lakini ilikuwa ni tofauti sana kwa Dkt. Justine ambaye yeye hakuweza kuonyesha hali yoyote ya masikitiko juu ya jambo lile. Dkt. Justine aliweza kulitafsiri jambo lile kwa haraka na kuhisi ya kuwa Boss France alikuwa akiwazia sana juu ya Vicky ambaye anaye alikuwa ni mgonjwa aliyelazwa hapo hospital bila ya hawa Esther na wengine kufahamu hilo. Hii ilikuwa ni siri kwa Dkt. Justine ambaye alifurahia ile hali na kuona yakuwa ingekuwa ni rahisi kwake kuweza kumpata Esther aliyekuwa amekwisha kumteka moyo wake mazima.

Esther alizidi kulia kwa uchungu huku akiwa amepiga magoti yake na kumsihi Dkt. Justine aweze kufanya lolote juu ya hali ya Boss France. Na hapo Dkt. Justine hakuwa na ubishi kwani hakutaka kuyaana machozi ya Esther yaendelee kumtoka. Alitoa maelekezo kwa madaktari wadogo na manesi kwamba ni nini wafanye ili kuhakikisha hali ya Boss France inahimarika mara moja. Ikabidi Dkt. Justine na Esther kutoka nje ili kuwapisha wahudumu kuweza kuhangaikia hali ya Boss France.

Dkt. Justine alikuwa akimgongagonga bega na kumpooza Esther kwa kumpapasa katika mgongo wake kwa lengo la kumtuliza kuacha kulia kwani hali ya Boss wake lazima ingeweza kuwa sawa kwa uangalizi wake. Aliendelea kumbembeleza Esther na kumsihi waelekee katika ofisi yake ili akapumzike,  Lakini ilikuwa ni tofauti kwa Esther ambaye hakuwa na haja ya jambo hilo. “Oooh!!! Bila shaka utakuwa haujala basi naomba tuelekee Restaurant kupata chakula pamoja” alizungumza Dkt. Justine ambaye alikuwa akishusha pumzi yake “Huuuh...”... huku akimtizama Esther kwa jicho la uchu wa kutaka kukubaliwa ombi lake. “Hapo umejiongeza kama mwanaume unayejitambua lakini asante nimeshiba na sihitaji chochote kwa sasa”.

Dkt. Justine alihisi kuishiwa na pozi kwani wakati Esther alipoanza kutoa jibu lake lilionekana kuanza kumpendeza na kumfurahisha lakini ghafla likawa na kona iliyoidhohofisha furaha yake. “Basi naomba twende ukapate chochote utakachokihitaji” alizungumza huku akitabasamu lakini majibu ya Esther.kwa mara nyingine hayakuweza kuuridhisha moyo wake “Sihitaji chochote kile Dkt. Justine” hayo ndiyo yaliyokuwa majibu ya Esther na yenye nyodo na ishara za dharau kwa Dkt. Justine.

 Esther alikuwa akiyafanya hayo yote huku akiwa na uhakika kwamba Dkt. Justine. asingeweza kumfanya chochote wala kushindwa kuacha kumsaidia Boss France kwa kuwa alikuwa akimpenda yeye. Ilikuwa imekwisha timia majira ya saa nane mchana  na baada ya kimya kidogo masikio ya Dkt. Justine yalisikia kupata ladha ya vanila katika ulimi wa mtu aliyetafuna mwarobaini, kwani Esther alikubali kwenda Restaurant pamoja na Dkt. Justine.

Furaha ilishamiri tena kwa Dkt. Justine na kuonyesha tabasamu kisha wakaanza kuelekea Restaurant. Lakini kabla hata hawajapiga hatua mbili tatu, Dkt. Justine aliitwa na mmoja wa manesi ambao walikuwa wakitoa matibabu kwa Boss France. Nesi huyo alikuja alipokuwa Dkt. Justine na Esther huku akikimbia na kuonekana kuwa mwenye furaha baada ya kuirejesha hali ya Boss France. Suala hilo lilikuja na taswira mbili kwani ilikuwa ni zaidi ya furaha kwa Esther ambaye aligeuka na kukimbilia kule alipokuwa Boss France huku naye Dkt. Justine akikimbilia huko huko ingawa moyo wake ulikuwa na manung'uniko kwani jambo lake alikuweza kufanikiwa na ndo kwanza lilikuwa katika hatua za awali.

Esther aliingia moja kwa moja mpaka kwenye chumba alichokuwemo Boss France bila ya kujali taratibu zozote na kwenda kumkumbatia Boss France aliyekuwa amekaa pale kitandani Waaaoooh!!!.. Iliendelea kuwa ni furaha isiyo na kifani kwani naye Boss France aliita Esther, Esther” baada ya kumuona kisha wote wakatabasamu huku machozi ya furaha yakimtoka tena Esther. Wakati hayo yakiendelea Dkt. Justine na wengine waliokuwepo pale walibaki kuwa mshuhuda wa tukio lile la kihisia.

Likini ghafla Boss France alikumbuka juu ya Vicky ambaye naye alikuwa amelazwa pale hospital ikiwa yeye mwenyewe ndiye aliyemleta hapo na kumahidi juu ya usalama wake na kila kitu kabla ya yeye kukumbwa na ajali. Mamaaa....!!!” Alikurumuka pale kitandani na kuchomoa drip aliyokuwa ametundikiwa katika mkono wake kisha akakimbia kuelekea katika wodi aliyolazwa Vicky. Kheeh!!!.. Ulikuwa ni mshangao na mshtuko kwa kila mmoja pale kasoro tu kwa Dkt. Justine ambaye alikuwa akifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea.

Boss France aliinia katika wodi aliyolazwa Vicky na kumkuta amesimama kwa kujiandaa kuondoka pale hospital huku akiwa pamoja na jopo la wale marafiki zake aliokuwa nao kule HAVOC NIGHT SPOT CLUB kabla ya kulazwa kwake hapo Hospital. Waooh!! Aliachilia simu yake aliyokuwa ameishika kutaka kumpigia Boss France na kumkumbatia Boss France kwa muda mrefu huku akiangua na kilio cha maumivu ya kupotezana na mbaya zaidi ni pale alipomwona Boss France akiwa na majeraha katika mwili wake.

Wakati huo Esther,  Dkt. Justine na lile jopo la madaktari na manesi lilikuwa likikimbilia huko huko huku Esther akiwa wakwanza. Baada ya kufika mlangoni na kutupa macho yake mbele alibahatika kumuona Boss France akiwa amekumbatiana na mwanamke ambaye alikuwa amegeukia upande wa pili na yeye kushindwa kumtambua. Looh!!!.. na hapo Esther aliendelea kulia kwa sauti huku akiita “Boss France,  Boss France”

MWISHO.

Je,  ni nini kitakachoendelea baada ya tukio lile la Esther la kumkuta Boss France akiwa amekumbatiana na mwanamke aliyeshindwa kumtambua kwa haraka?

Endelea kuwa nasi katika sehemu zinazoendelea.

 


MWANDISHI

SEBASTIANI SEBA

PHONE: 0746445197

WHATSAPP GROUP 


 

Post a Comment

0 Comments