SEHEMU YA KUMI NA TATU
Ilikuwa ni saprize nzito
naya aina yake ndani ukumbi wa kikao na kila mmoja asiweze kupata picha
varanguti ambalo lingeweza kutokea hata Boss france mwenyewe alihisi ni kama
ndoto.
Samahani Vicky naomba
utoke nje ya ukumbi wa kikao. Boss
france alimtaka vicky kusubiri nje mpaka
kikao kitakapokwisha kwa maana isingeweza kuleta picha nzuri kwa
wafanyakazi wenzie, ilihali alikuwa akitambua taratibu zote na uzito wa kikao
kile.
Vicky hakutaka kujibu
chochote kile kwani ilimbidi kufanya kile alichoamuriwa na Boss wake. Alitoka
nje ya ukumbi wa kikao ingawa nafsi yake haikuridhia kwa kuhisi kama kitendo
kile kilichofanywa na Boss wake kilikuwa nicha kumuaibisha kwa haiba iliyokuwepo
pale ndani.
Sidhani kama ni dhamira
yake nahisi amefanya vile tu kwa sababu ya uoga wa awara wake. Vicky alijisemea huku mishipa ya ghadhba ikimpanda taratibu
Wakati huo ndani ya
ukumbi wa kikao kilichokuwa kikielekea tamati. Kasheshe zilitaka kuibuka baada
ya Esther kujikuta akichekelea kile kilichomkuta Vicky. Kitendo hicho kilichoonekana
sicho cha kiungwana kilimfanya Boss france kuanza kupaniki na kuuliza kwa
hasira.
Kitu gani
kilichokuchekesha Esther? Mapigo ya Esther yalishtuka kidogo na fahamu zake kuweka
umakini. Mmmh! Hapana Boss mimi sijacheka ila nimefurahi kwa kuona umefanya
maamuzi ya Busara kwa kutambua taratibu za kikao chetu.
Esther alitoa jawabu
zuri lenye uwezo wa kuzichanga karata kwa kutumia macho, naye Boss france
alijikuta akiwa mpole kama mboga iliyokosa matumizi ndani ya mgahawa.
Kikao kilifikia tamati
na Boss france aliwaomba wafanyakazi wote kurejea katika ofisi zao na kuendelea
na majukumu. Wote walianza kutawanyika na kuelekea katika maeneo yao ya kazi
lakini wazee wa mbaga walikuwa wa mwisho kutoka pale ukumbini kwa kuhisi kwamba
pengine kungeweza kuwa na kikao baada ya kikao.
Nilitegemea kuona marudio
ya lile pambano la vitasa kati ya Twaha kiduku na dullah mbabe hahahaa... Bwana jeshi alilianzisha huku kicheko kikimpalia
Msodoki: Mimi nilijiandaa kuwa refa ili niweze kufaidi vingi kwa
ukaribu. Wote walicheka huku Bwana kichuya akiwasihi wenzie kuelekea ofisini mwao
kwani siku hiyo alianza kuonekana mbaya baada ya uwanja kuonekana umeinama.
Baada ya Boss France
kutoka nje ya ukumbi wa kikao akakutana na Vicky akiwa amesimama kwa masikitiko
nje ya mlanago. Alimvuta mkuku mkuu hadi ofisini kwake na bila ya kujali kuwa
Vicky alikuwa bado hajapona vizuri.
Niache tafadhali hakuna
mbuzi wala punda hapa wa kumpeleka peleka hovyo kama unavyotaka. Vicky
aliongea kwa hasira na kwa uchungu huku akiendelea kuvurutwa mpaka ndani ya
ofisi ya Boss france pasipo kuelewa Boss France alikuwa na lengo gani.
Naomba niache tafadhali,
achana na mimi. Mbwa wewe usiyekuwa na huruma wa haya. Looh! Kauli hizo
za Vicky zilizojilimbika kashfa na dhihaka kwa Boss wake hazikuweza kufua dafu
kwani alijikuta akiambulia kibao kizito kilichosikika kama gari lililokumbwa na
pancha.
Paaah! Mwanamke mshenzi sana wewe, usitake kuniharibia siku yangu wewe ni
wakunitukana mimi kwa hadhi ipi uliyonayo. Boss
france alijikuta akifanya maamuzi ambayo hakuwahi kuyataraji katika maisha yake
pengine jambo hilo lingemjaza wimbi la majuto hapo baadae.
Wakati hayo yakiendelea
ndani ya ya ofisi ya Boss france. Bwana jeshi, Msodoki na Bwana kichuya nao
walikuwa wakija katika eneo la ofisi ya Boss france ili kutaka kujua nini
kilichoweza kutokea baada ya kusikia kibao kile na sauti za malumbano baina ya
Boss France na Vicky.
Walifika nje ya ofisi
ya Boss ya Boss France na kusikia sauti ya Vicky akiwa anajlia, nao waliendelea
kubishana kwamba ni nani kati yao angeweza kujilipua kugonga mlango ili
waingine ndani.
Eeeeh! Esther naye huyo anakuja nadhani atakuwa amesikia lile
bomu lililokuwa limelipuka humo ndani. Bwana jeshi alizungumza maneno yake yaliyokuwa yamejaa mizaha
kama ilivyokuwa kawaida yake lakini Msodoki alimsihi kuacha masihara na kungalia
namna ya kufanya kilichowavuta mpaka pale.
Mimi nafikiri tumsubiri
Esther ili tuingie naye maana naona kama
anakuja uelekeo huu. Yalikuwa
ni maneno yenye busara na hekima ndani yake ya Msodoki. Wote walikubaliana na mawazo
hayo na kuendelea kusubiri.
Jamani kuna nini
kimetokea ndani ya ofisi ya Boss? eti mbona kama sielewi elewi au Vicky kalizua
tena. Esther aliwasili eneo walipokuwa wakina Bwana jeshi na wenzake nakuuliza
maswali ambayo hayakuweza kupata majibu yoyote.
Alishtuka na kujiziba
mdomo wake mara moja baada ya kusikia sauti ya kilio cha Vicky ndani ya ofisi
ya Boss france. Papo hapo akaanza kugonga mlango na kuingia ndani pasipo
kuruhusiwa. Nalo kundi la wanambaga lilijiunga na kuwa sehemu ya msafara wa
Esther kisha wakaingia ndani
Vicky, Boss jamani
kuna nini mbona hivi? Kila
mmoja aliuliza swali ambalo halikuweza kujibiwa. Kitendo cha Esther kumkuta Vicky
akiwa amekaa chini, kashika tama na kujiinamia huku machozi yakimtiririka kwa
maumivu, kilimfanya aingiwe na moyo wa huruma kiasi cha yeye kuhisi maumivu
aliyoyapata Vicky licha ya tofauti na chuki walizokuwa nazo.
Wakati huo Boss france
alikuwa amekaa kwenye kiti chake na kuinamia meza kiasi ambacho kiliweza
kuufanya uso wake kujificha. Esther
aliendelea kumbembeleza Vicky na kumtaka
asiendelee kulia kwani jambo hilo lilimpelekea Esther naye kulengwa lengwa na
machozi.
Bwana kichuya
alimsogelea Esther na kumnong’oneza sikioni mwake kwamba angependelea kumuona akifanya
mazungumzo na Boss France pengine ingeweza kuwa rahisi kujua namna ya kukabili
madhila yaliyoweza kujitokeza na kazi ya kumbembeleza Esther ingewafaa sana wao.
Sawa nimekuelewa vizuri
nadhani ni jambo zuri na lenye busara na ukizingatia kesho tuna safari ya
kwenda Zanzibar hivyo tunapaswa kulimaliza hili mapema ili kila mmoja aweze
kuwa na amani. Esther alikubaliana na maneno ya bwana kichuya wakati huo
bwana jeshi hakuwa mbali na Vicky.
Esther alisogea karibu
na Boss france aliyekuwa ameinamisha kichwa chake juu ya meza na kuwa kimya kwa
wakati wote tangu ujio wa akina Esther ndani ya ofisi yake. Boss, Boss,
Boss... Esther alimuita Boss France mara tatu tatu huku mkono wake wa kulia
ukilazimika kupapasa kichwa cha Boss france. Aliendelea kumsihi Boss wake kwamba
angejaribu kuzungumza ili waweze kuyaweka mambo sawa huku akimkumbusha juu ya
safari yao ya siku ya kesho kwenda Zanzibar.
Mmh! Amenikosea sana
ila namuachia tu Mungu. Boss france alianza kufunguka kwa sauti ya chini chini na kuzidi
kutoa manung’uniko yake juu ya Vicky kwamba ndiye aliyeweza kusababisha yote
hayo.
Mara ghafla Vicky naye
alikurupuka kwa hasira baada ya kusikia Boss france akimtupia lawama zote juu
ya kile kilichoweza kutokea. Yaani tena bora ukae kimya kabisa, kati ya
mimi na wewe nani aliyemkosea mwenzake, unawezaje kunipiga kibao kizito kama
kile ilihali unafahamu yakuwa mimi bado ni mgonjwa, huo ni utu kweli? Yaan...
ooh! Vicky aliongea kwa uchungu huku akizidi kumwaga machozi
ya hasira
Yalaaah! Bwana
jeshi aliamua kudakia baada ya kusikia maneno yale kutoka kwa Vicky kwani
yalimgusa sana katika ubongo wake. Ndio maana tulisikia kitu kizito kama
vile mlipuko wa bomu, Daah! Kumbe kilikuwa ni kibao aseee! Hii haijakaa
sawa kabisa ama mnasemaje wenzangu? Bwana jeshi alitoa yake ya moyoni
ingawa alijificha katikati ya kivuli cha wenzie na kisimtoshe kumsitiri. Wote walikubaliana
na kauli ya Bwana jeshi lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kutoa sauti yake nje
bali walitikisa tu vichwa vyao kwa sababu Boss France hakuweza kuwaona kwa
wakati huo. Mara ghafla Boss france akakurupuka na kusimama kama upepo wa
kisulisuli. Tafadhali Bwana jeshi naomba ukae kimya tena ikibidi utoke
ofisini kwangu. ilikuwa ni wazi kwamba Boss france hakupendezwa
na kauli za Bwana jeshi, kauli hizo zilipenya vilivyo katika ufahamu wa Boss
france kufanya kazi dizaini ya kumtoa mlevi ndotoni.
Ama kweli “mkuki
kwa nguruwe kwa binadamu mchungu” Bwana jeshi hakuwa na budi
kutoka nje lakini baada ya muda mfupi wote waliokuwepo ndani walau walifikia
muafaka mzuri na kila mmoja kuanza kutawanyika. Vicky alipewa ruhusa ya kwenda kupumzika
nyumbani kwake na mara moja aliondoka hapo bila ya kusema chochote baada ya
ruhusa aliyopewa na Boss France.
Ikiwa ni mda mchache
baada ya Vicky na wengine kuondoka ndani ya ofisi ya Boss France.
Kilichoendelea kuusumbua ubongo wa Boss France kilikuwa ni majuto ni mjukuu
kwani aliwaza na kuwazua sana juu ya kili kichoweza kutoea. Aaah! Mbona
kama nimeikosea sana nafsi yangu, imekuaje leo nimefikia maamuzi haya juu ya
Vicky. Mwanamke ambaye nilishaanza hata kumpenda, leo imekuwa hivi? Hapana,
hapana kabisa nahisi kuna mtu kaniloga.
Boss france aligonga
meza na kushusha pumzi zake huku akijutia sana juu ya kilichotokea kati yake na
Vicky. Aliona hakikuwa kitendo cha busara cha yeye kufanya vile, alijihisi
kwamba yeye ndiye aliyekuwa na makosa na hasira zake ndo zilizoweza kumponza.
Ofisini kwake
hapakuweza kukalika na maana kila jukumu la kiofisi alilojaribu kulifanya
lilikuwa gumu kwako siku hiyo. Aliwaza nini angeweza kufanya Ooh! Nafikiri
nami ningeenda kujipumzisha tu nyumbani na kufanya maandalizi ya safari ya kesho.
Alitoka ofisini mwake na kuelekea kwenye
ofisi ya sekretari wake Esther ili aweze kumuaga. Lakini Esther naye alikuwa
akija katika ofisi ya Boss France.
Yes Esther, ulikuwa ukija katika ofisi yangu? Esther aliitikia abee Boss
Boss france: Vipi kuna jambo jipya la kikazi? maana naona kama vile
kichwa changu hakiko sawa.
Esther: Usijali, nilitaka tu nikushauri kwamba ni vema ungeenda
kupumzika na kujiandaa na safari ya kesho.
Boss France: Ohooh! Hata na hivyo nilikuwa nikija kukuaga
Esther: Basi sawa, alafu ticket zetu zimeshakuja, tutasafiri na
usafiri wa majini kwa Boti ya Azam Marine inayoondoka saa sita.
Boss France: Sawa kabisa, usafiri wa majini utafaa zaidi walau hata
kuweza kurefresh macho kidogo. Kisha akacheka hahahaa. Boss
france alijitahidi kuongea kama vile alikuwa ameshasahau mambo yote yaliyoweza
kutokea masaa machache hapo nyuma kwani aliongea akiwa na uso uliojaa furaha na
tabasamu.
Esther: Basi ngoja nikuletee ticket yako
Boss France: Hahahaaa Esther, hapana usisumbuke kwenda ofisini. Safari
yetu ni moja hivyo kaa nazo tu hamna tatizo
Esther: Sawa Boss nimekuelewa, uwe na muda mwema. Esther mrembo
mwenye madaha hakusita kumgusa kidogo bega Boss wake wakati akimuaga na
akaondoka kuelekea ofisini kwake.
Boss france alipiga
hatua moja na kugeuka tena upande aliokuwa akielekea Esther na kuongeza neno. Esther
Aaamm hakikisha nawe leo unaondoka mapema ili kujiandaa na safari. Sawa Boss usijali. Esther alisimama
kidogo akajibu kisha akaendelea na mwendo kuelekea ofisini mwake.
Boss france aliondoka
na kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwake Oyster bay Lakini kiuhalisia
akili yake haikuwa sawa kabisa siku hiyo toka alipovurugana na vicky. Ilimbidi
asogeze gari pembeni ya barabara kisha akasimama. Alifanya hivyo kwa lengo la
kuwasiliana na Vicky ili amuombe msamaha kwa kile alichokifanya kwa sababu moyo
wake haukuwa na amani kabisa.
Aliamua kumpigia simu Vicky
lakini simu yake iliita tu pasipo kupokelewa. Akajaribu tena mara ya pili naya
tatu lakini mambo hayakuweza kubadilika kwani simu haikupokelewa. Alijishika
tamaa na kufikiri kidogo kisha alipata wazo kwamba ingefaa kumuandikia ujumbe
wa simu
Hello! Vicky, kiukweli
nimejaribu kukaa kimya lakini nimeshindwa kotokana na kile nilichokufanyia, Moyo
wangu hauna amani kabisa ya kufanya chochote kile kwani nakiri na kujutia kosa
langu. Ila usisahau yakuwa mimi ni binadamu na nimeumbiwa udhaifu hivyo naomba
unisamehe sana Vicky. Wakati huo Vicky hakuwa mbali na simu yake kwani
alishuhudia yote tangu Boss France alipokuwa akimpigia. Lakini baada ya SMS
kuingia katika simu yake aliona siyo mbaya kujaribu kuisoma labda pengine
ingeweza kumshawishi.
Haaaaaa! Vicky alishusha
pumzi na kunywa glass moja ya maji. Ilikuwa ni wazi kuwa ujumbe ule wa simu
kutoka kwa Boss France uliweza kumshawishi. Akili yake ilikubali kumsamehe Boss
France ingawa mwili wake haukutaka kujishughulisha kujibu ujumbe ule.
Boss france alizidi
kujisikia vibaya baada ya kuona kimya lakini taswira ya rafiki yake Meneja
Tinno ilimjia machoni pake na kukumbuka yakuwa wote walipaswa kusafiri siku ya
kesho kuelekea zanzibar. Mara moja alinyanyua simu yake na kumpigia
Tiiiiiiii....
tiiiiiii.... tiiiiii..... simu
iliita kwa muda kidogo kisha ikapokelewa
Meneja Tinno: Naam Boss wa maboss
Boss France: Yes
Meneja Tinno: Vipi rafiki yangu, mbona kama kinyonge tena?
Boss France: Aaah! Nahisi kama siko sawa vile, then kuna jambo
natamani tuweze kulizungumza siku ya leo tukiwa ana kwa ana.
Meneja Tinno: Sawa haina shida, na mimi najiandaa hapa kutoka kazini.
Hivyo sijajua tutakutaniana wapi vile?
Boss France: oooh! Nadhani ingekuwa vema kama ungepanga wewe Boss
Meneja Tinno: Eeeeh! Mmmh! Vipi pale HAVOC NIGHT SPOT CLUB naona
kama kumekaa vizuri kwa hadhi yetu
Boss France: Mmmh! Pale sawaa lakiniii... sidhani kama patatufaa zaidi,
maana kuna tatizo lilishawahi kutokea pale siku za nyuma kidogo. Hivyo tungepata
sehemu nyingine tofauti na hiyo.
Meneja Tinno: Basi tukutane New maisha club muda wa saa tatu.
Boss France: Hapo sawa, bila shaka tutaendelea kuwasiliana
Meneja Tinno: Ok, ok
Boss France na meneja
Tinno walifikia makubaliano kwamba ni wapi wangeweza kukutana hapo baadae kisha
Boss France aliendesha gari kuelekea nyumbani kwake.
Ilikuwa imeshatimu
majira ya saa tisa alasiri na kenda na alitumia mda usiopungua nusu saa hadi
kufika nyumbani kwake.
Piiii... piiii...piiii... sauti ya honi ililia ili geti liweze kufunguliwa ikiwa
ishara tosha kwamba Boss France alikuwa ameshafika nyumbani kwake
Aaaaah... Boss mwenyenye, hahahaa karibu sana. Malila mwanajogini alipokea begi la Boss wake ambaye
alikuwa akiishi naye kama ndugu na kama sehemu ya familia yake maana Boss
france hakuwa na mke wala mtoto hata mmoja licha ya kuishi katika mjengo mkubwa
nawa kifahari.
Boss France: Ahsante, bila shaka utakuwa umeshinda salama.
Malila mwanajogini:
Ndiyo mkuu, vipi majukumu?
Boss France: aaah! Kheri kabisa, sasa malila mimi naingia ndani ila
badae nitatoka mida ya saa mbili na nusu hivi
Malila mwanajogini: Sawa Boss, mimi ni nani mpaka nikupinge
Boss France: Hahahaaa, acha habari zako. Then angalia ndani ya begi
kuna zawadi yako huko
Malila mwanajogini: Daah! Asante sana Boss wangu, Mwenyezi Mungu akuzidishie
kila uchao.
Boss france aliitikia haya
huku akielekea ndani. Alisogea karibu na friji akavuta kinywaji cha juisi ya
embe na kukimimina mdomoni haraka haraka.
Yani leo sijala kabisa
alafu sihisi hata njaa, basi nitakuwa nimeshiba. Alijiuliza swali na kujijibu kisha akaelekea chumbani mwake.
Alijiangusha kitandani bila hata ya kuvua viatu na kama mzaha vile wimbi zito
la usingizi likamchukua.
Boss france alilala
fofofo kwa masaa kadhaa kutokana na uchovu aliokuwa umemjaa siku hiyo.
Muda ulisogea na kufika
mpaka saa mbili na nusu usiku lakini Boss france alikuwa bado yupo usingizini.
Wakati huo malila
mwanajogini alikuwa sebuleni akitizama taarifa ya habari. Heeheh! Mbona kama muda umeenda lakini
sioni dalili yoyote ya Boss kutoka ndani. Malila mwanajogini alijihoji
baada ya kuona kimya kirefu na muda ukizidi kwenda. Ikabidi asogee karibu na chumba
cha Boss France na kugonga mlango.
Ngo, ngo, ngo,... ngo,
ngo, ngo.
Boss France alishtuka
kutoka usingizini huku akilambalamba midomo yake na alipotizama saa yake ya
ukutani ilikuwa imeshatimia saa mbili na dakika arobaini. Na hapo usingizi wote
ulimuisha akadogea hadi mlangoni.
Aaaaah! Ooooh! Alijinyoosha
na kupiga mihayo mingi kisha akafungua mlango
Boss France: Alaaah! Vp malila
Malila mwanajogini: Safi Boss, muda umekwenda uliniambia utatoka au
umeghairi.?
Boss France: Hapana, nilikuwa nimesinzia kidogo ila asante kwa
kunikumbusha.
Malila mwanajogini: Sawa mkuu
Malila mwanajogini
alirudi sebuleni kuendelea na taarifa ya habari naye Boss France alivua nguo
zake za kazini, akafunga taulo, akachukua mswaki wake na kuingia bafuni mara
moja. Aliswaki na kuoga bila ya kupoteza nyakati akarudi chumbani mwake na hapo
ilikuwa imekwisha timu saa tatu kamili
Ahahaa! Asee... Niko
nje ya mda kweli.. na ndugu yangu huwa yuko vizuri sana kwenye kuzingatia muda
ilihali mimi ndiye niliyemualika.
Alivaa haraka haraka
mavazi yake ya ujana na kutupia bareti kichwani bila ya kusahau kujinyunyuzia
unyunyu wa Kifaransa kisha akabeba simu yake na kutimka nje.
Malila njoo ufunge geti
ndungu yangu usiku huu. Boss
france alinyooka mpaka getini, akalifungua na kurudi kwenye gari kisha akatimka
mara moja kuelekea New maisha club walipopanga kukutana na Boss
france. Wakati huo naye Meneja Tinno alikuwa akimpigia simu Boss france ambaye
hakusita kuipokea.
Boss France: Yes Boss,
nipo njiani nimekaribia kufika.
Meneja Tinno: Ohooh!
Sawa nimekupigia mda sana lakini simu iliishia kuita tu.
Boss France: Daah!
Samahani sana, yaani huwezi amini tangu nimefika nyumbani hapa ndo ninashika
simu kwa maana nilikuwa nimelala
Meneja Tinno: Basi sawa usijali. Mimi nimeshafika hapa nakusubiri
Boss France: Ok, chapu mara moja nitakuwa hapo
Meneja Tinno: Sawa.
Boss France alikanyaga
mafuta haswa ili kuwahi ndani ya viwanja vya New maisha club. Ilimgharimu
kiasi cha muda wa dakika 20 tu kuweza kufika hapo.
Alishuka kwenye gari,
akaweka loki na kuelekea ndani. Nje ya mlango wa kuingia ndani ya New
maisha club alikutana na mabamnsa waliokuwa wamesimaama kama mibuyu ya
kale ya Mpwapwa. Lakini kwa muonekano wake wa kipedeshee hakuweza kupata
kizuizi chotete kwani alipitiliza moja kwa moja hadi ndani.
Palikuwa pameanza
kuchangamka ndani ya New maisha club kwa kuchagizwa na midundo
mikali pamoja na taa zilizowakawaka kama vile vimulimuli. Alitizama kushoto na
kulia, juu na chini nakwa bahati nzuri alibahatika kumuona Meneja tinno akiwa
upande wa juu wa VIP.
Alitembea mpaka eneo la
kaunta alilokuwa amekaa Meneja Tinno ambaye alining’iniza miguu yake kwenye
kiti cha kuzunguka huku akipata kinywaji baridi.
Boss France alisogea
karibu kabisa na kumshika begi Meneja Tinno.
Aaah! Boss la maboss,
karibu sana. Karibu kiti ndugu yangu. Meneja Tinno alimkaribisha Boss France kwa mbwembwe kweli
kweli na wakati huo kinywaji nacho kilianza kumpanda kichwani kwani alikuwa
amefika mapema kabla ya Boss france.
Boss france alimshukuru
Meneja Tinno lakini alimuomba wangehamia kwenye meza, ili wawili hao waweze
kujadili mambo yao.
Basi sawa tusogee meza
ile iliyokaribu na ukuta. Meneja Tinno aliendelea kwa kusema
Waiter naomba nisogezee
hivyo vinywaji vyangu huku. Meneja
Tinno alikuwa na dalili za kuvaa miwani na hata yeye mwenyewe alianza
kujishtukia. Ikabidi ayagubike mdomoni kwa pupa maji yake makubwa aliyokuwa
ameyashika mkononi.
Wakati huo waiter
alikuwa akileta vinywaji naye Boss Tinno alikuwa akimkata jicho vilivyo.
Karibuni sana Maboss. Waiter alimsogelea Boss france na kumuuliza. Nikuletee
kinywaji gani Boss?
Ahahaah! Niletee Maji
makubwa tu kwa sasa.
Looh! Meneja Tinno
alidakia. Hapana, hapana naomba umletee Hennesy huyu ni mtu mzito sana hapa
mjini hahahaa...
Boss france naye
aliishia kucheka na kusema Sawa lete kashasema Boss. Ulikuwa ni urafiki mzuri sana kati yao kwani
walikuwa ni watu walioelewana sana.
Pasipo kupoteza muda
Boss france ilibidi aanze kuweka mezani agenda iliyoweza kuwakutanisha.
Ndugu yangu utanisamehe
sana, maana siku ya leo sijachangamka kiivyo kwa sababu kuna mambo hayajaenda
sawa kabisa. Naye Meneja Tinno
alidakia tena Mmh! Embu ngoja ni mambo gani tena hayo? Maana kama ni pesa
unazo za kutosha wala sina shaka katika hilo, Mmmh! Umefiwa labda. Hapana
hapana sidhani au ni mambo ya mahusiano nini ndugu yangu mapenzi
mahabuba,habuba huko?
Boss france alicheka.
Hahaaa dah! Hapana ndugu yangu. Umenilimbikizia mambo mengi sana. Hayo yote
siyo ila jambo lenyewe liko hivi.
Boss france hakuwa na
budi kuanza kumsimulia Boss france madhila yote yaliyoweza kumkumba siku hiyo ofisini
kwake.
Wakati huo waiter naye
alikuwa akileta vinywaji vya Boss france. Aliviweka mezani na kumkaribisha Boss
france huku akitabasamu.
Looh! Nguo
yake fupi iliyaachia mapaja yake yote nje na kuanza kumchanganya Meneja Tinno
aliyeanza kuchangamka.
Hivi Mrembo uliniambia
unaitwa nani vile? Meneja Tinno
aliuliza
Naitwa Fetty.. aaam..
Featty Mtakuja Boss.
Mrembo yule alimjibu Meneja Tinno
Aaah! Sawa Fetty, basi
chukua kiasi hiki nawewe upate kinywaji mrembo. Meneja Tinno alitoa wallet yake na kuvuta kiasi cha Elfu
hamsini kisha akampatia Fetty
Eeeh! Wow! Asante sana boss
Meneja Tinno
akaendelea. Basi sawa nitakuona badae, kuna mambo naweka sawa hapa na ndugu
yangu.. na fetty mtakuja aliitikia sawa Boss. Kisha akaelekea
kaunta.
Mrembo fetty aliembea
kwa madaha sana naye Meneja Tinno aliongezea neno juu ya fetty
Aseee! Kweli wewe ndo fetty mtakuja na tutakuja tu mamaa siyo kwa
mshepu huo, cheki na mwendo wake alaaah! Hahahaa
Alipomaliza ya Fetty
akamgeukia Boss france na kumwambia. Ndugu yangu usijali tuko pamoja,
nadhani hakijaharibika kitu? Naye Boss France alimjibu ni sawa kabisa
naona tupo pamoja kisha akacheka na wakaendelea na mazungumzo yao.
Meneja Tinno: Ndugu yangu usiogope, wala usiwe na shaka
kabisa kwa yote yaliyokukuta sababu ni mambo ya kawaida sana kwa sisi binadamu.
Boss France: Ni kweli kabisa ndugu yangu nimekuelewa.
Meneja Tinno: Sasa hivi wewe waza zaidi juu ya kikao chetu na safari
yetu ya hapo kesho.
Boss France: Sawa kabisa, alafu vipi kuhusiana na yule mrembo Zeyna?
Meneja Tinno: Yule yupo na usijali na tutakuwa naye kwenye kikao
Zanzibar.
Boss France: Sawa kabisa hapo umenena
Meneja Tinno: Yule ni sawa na kuku wako, sasa manati yanini, embu
tuendelee kupata vitu
Waiter tuongezee
vinywaji. Maneno na ushauri wa Meneja Tinno ulimpa nguvu sana Boss France na
kusahau yote kwa wakati huo na zoezi kubwa likawa ni mwendo wa kunywa tu.
Walikunywa kiasi kingi
cha pombe za wine na hatimaye Boss France ndiye aliyekuja kuibuka bingwa kwenye
dizaini hiyo ya shindano la kunywa. Macho yake yalianza kuona mawenge, mawenge
na kila aliyepita au kumuona mbele yake alihisi ni mrembo.
Baada ya muda kidogo alikurupuka
na kusema. Nakuona mrembo Zeyna.
Meneja Tinno alishtuka
na kugeuka nyuma akifikiri yakwamba Boss France alimuona Zeyna lakini hapakuwa
na Zeyna wala picha ya Zeyna.
Meneja Tinno: Zeyna yuko wapi?
Boss France: Mbona nimemuona hapa muda huu au ilikuwa ni wewe.
Meneja Tinno: Hahahaa ushalewa wewe, kilichobaki ni kuondoka tu hapa.
Meneja Tinno alisimama na
kuwaza namna ya kuondoka na Boss france kutokana na hali kunywa kupitiliza
kwanj ilikuwa ni ngumu kumuacha Boss France aondoke peke yake.
Wakati hakifikiri hilo akili yake kwa upande mwingine ilifikiri kuhusu Fetty na akose la kufanya. Aliingiza mkono mfukoni ili kutoa funguo yake ya gari lakini hakuweza kuiona. Alishtuka na kuendelea kujisachi kila upande wala hakuweza kuiona akabakia kushangaa huku akiwaza ni wapi alipoiweka.
***MWISHO***
"ENDELEA KUFUATILIA
MIENDELEZO YA TAMTHILIYA YA PESA ZA SHEMEJI KILA SIKU YA JUMAMOSI PIA USISAHAU KUTIA COMMENTS ZAKO HAPO CHINI"
NCHI YETU, TAMTHILIYA YETU, FURAHA YETU. PESA ZA SHEMEJI ON AIR
“KAMA ELIMU YETU ISIPOTUOKOA, BASI VIPAJI VYETU VITUOKOE”
EEH! MUNGU BABA TUSAIDIE.
MWANDISHI: SEBASTIAN S MASABHA

0 Comments