PENZI LA MASHAKA
A STORY SCRIPT
BY
SEBASTIAN S. MASABHA.
0758-162527
SEHEMU YA PILI 02.
EXT: SEBBY ANAKAMATA SPANA NA KUANZA
KUSHUSHA INJINI YA GARI.
SEBBY.
Dah! Hii ngoma nzito kweli kweli. Yaani hizi
kazi za kuvamia huwa ni kipengele. Mtu unasomea jambo A unakuja kuhangaika na
jambo B. tofauti kabisa na uhalisia.
{Sebby anashtushwa na ujio wa Konki ambaye
anamgusa Sebby begani}
KONKI.
Vipi chafu yao, mbona unalonga mwenyewe
asubuhi, asubuhi. Shida
nini au ndo mastresi ya maisha?
SEBBY.
Aah! Wapi konki, maisha
si ndo hayahaya tu mzee.
KONKI.
Sema bora yenu nyinyi
mlioenda hata maskuli, maana mkipata gepu mchezo unageuka chapu kwa haraka.
SEBBY.
Sidhani mzee wangu, siyo
kwa karne hii, labda Mungu atende miujiza.
KONKI.
Sema kweli, ila mimi
naamini utatoboaga tu huko mambele, Jah atablesi.
SEBBY.
Shukrani buda, tuzidi
kuombeana tu. Sema nini Konki embu nielekeze jambo kidogo hapa kwenye hii
injini. Sijui kuna nati sijaifungua ama vipi.
KONKI.
Poa chafu yao, alafu leo
Red vipi mbona sijamsoma mpaka sasa.
SEBBY.
Asee.. mwamba jana si kaguswa kidole na “Nge”
{Wakati Sebby na Konki wakiendelea na
majukumu pamoja na maongezi yao. Anaingia Master gereji na vijana wake wengine}
MASTER.
Sasa chafu yao, wewe na masuala ya kutengeneza
injini ni wapi na wapi. Nenda kazibe pancha kwenye lile gari jeupe. Hizi kazi
zina wenyewe bhana.
{Sebby aliyefahamika kwa jina la chafu
yao pale gereji, alikubali kwa kitikisa kichwa na kusimama kinyonge kwenda
kufanya shughuli ya kuziba pancha ya gari jeupe}
MASTER.
Haya kila mmoja achakarike na sehemu yake
sitaki vijana wazembe hapa, alafu tuje kusumbuana mda wa kukatiana jax (pesa).
Yaani sitaki kabisa.
WOTE.
Sawa master tumekuelewa. Sisi ni nani hasa
hadi tukupinge.
{Master gereji alikuwa ni moja ya watu
wenye kupenda sifa, kuogopwa na kuheshimiwa kila mara kitendo ambacho kilikuwa
kikiwanyima wafanyakazi wengine uhuru na kukaa vikundi kumsimanga}
Fade out
NJIRO NYUMBANI KWA KINA SABRINA (ASUBUHI)
{Sabrina msichana anayeishi maisha ya
kishua anajaribu kutafakari na kujiuliza endapo kama kuna tofauti yoyote
iliyojitokeza baina yake na Sebby}
SABRINA.
Hivi ni kitu gani kibaya nilichomfanyia
sebby? Maana amebadilika ghafla tu, ona sasa hata sms zangu hataki kujibu.
{Mawazo ya Sabrina yanakosa majibu sahihi
na subra. anaamua kumtumia Sebby ujumbe mwingine}
(Sabrina sms)
“Hey! Sebby mbona umechange sana now days, kama
kuna kitu nimekukosea si bora uniambie maana nashindwa hata kukuelewa. Anyway naomba
unijibu tafadhali”
{Ujumbe alioutuma sabrina unaonyesha kupokelewa
na Sebby hivyo sabrina anashusha pumzi zake na kusubiria kwa hamu reply kutoka
kwa Sebby}
(Sebby sms)
“..............................................................................................”
{Sabrina akiwa amejilaza kitandani.
Anaamua kuyakimbiza macho yake kwenye simu baada ya kusikia mlio wa sms}
SABRINA.
Camong! Huyu mwanaume ananitumia sms hewa. OMG!
What is this?
{Sabrina anashtuka na kuchukia baada ya
kupokea sms hewa kutoka kwa Sebby. Lakini kwa sababu anampenda, haishii hapo
bali anaendelea kufikiri ni kipi kingine cha kufanya}
SABRINA.
Jamani huyu Gentleman
mbona ananifanyia hivi si ataniuwa kwa presha. Au nimtumie Sms nyingine?. But
no.... atazidi kuniumiza coz atahisi
nampenda sana. Eeeh! Ngoja nimpigie simu.
{Sabrina anaona njia nzuri ya kupata majibu
sahihi na kuutuliza moyo wake ni kumpigia Sebby}
SABRINA.
Yani huyu mwanaume sijui
amekuaje, mbona simu yake inaita tu hata hapokei.
{Sabrina anajaribu
kupiga tena simu huku akiwa na shauku kubwa ya simu yake kupokelewa}
SABRINA.
Jamani mbona hivi,
ananifanyia makusudi au ndo ubize. Camong Sebby.
{Sabrina anachukia
na kuirusha simu yake kisha anajilaza kitandani baada ya Sebby kutopokea calls
zake}
Fade out.
GETONI UNGA LIMITED ( ASUBUHI)
INT. RED ANAAMKA KITANDANI.
{Red anaamka baada ya kumulikwa na mwanga
wa jua uliokuwa ukipita katika upenyo wa dirisha}
RED.
Tobaa... kumbe kumeshakucha kiasi hiki wacha
niamke kwanza alafu mafaili yatajipanga yenyewe kichwani.
{Kabla ya kufanya chochote kile Red anaangalia
mkono wake kwenye sehemu aliyong’atwa na “Nge” usiku wa mawio hiyo}
RED.
Hapa mbona safi tu. Ila
ngoja kwanza nikalambe supu yetu ya mtaa kwa mama mboksinyo alafu mafaili yataendelea
kujipanga yenyewe kichwani.
{Red anatoka nje
kuelekea mgahawani huku mswaki wake ukiwa mdomoni na mkono wake ukibeba
kijichupa cha maji}
Fade out
MGAHAWANI (PAMBANA NA HALI YAKO MGAHAWA)-ASUBUHI
INT. RED ANAINGIA MGAHAWANI.
{Red anaingia mgahawani huku akipokelewa
kwa mbwembwe na mama mboksinyo pamoja na baadhi ya marafiki zake}
MAMA MBOKSINYO.
Oyoooo...! Chali wa mapesa, chali wa kuvunja ndo
huyo sasa anaingia mjengoni
RED.
Kausha basi Bi mdashi. Mbona unanukia wenge
kama vile umemuona bakhresa kumbe kapuku mmoja tu.
MAMA MBOKSINYO.
Ahaah! Red kwa hiyo unanitolea nje siyo
RED.
Siyo nakutolea nje, tatizo lako uko resi sana
yaani kelele nyingi wewe mama. mara mjengo, mjengo kuna mjengo hapa au
kijimgahawaha tu.
{Mama mboksinyo mmiliki na muuza mgahawa
wa pambana na hali yako anambadilikia Red ghafla baada ya kuona wanapishana
lugha}
MAMA MBOKSINYO.
Embu tuyaache hayo maana ushanikasirisha Red.
Kwanza nakudai buku, jana umekuja hapa umekula na kuondoka na mihogo bila ya
kulipa.
RED.
Aaah! Bi mdashi ina maana wewe haujawahi
kutaniwa?. Mimi na wewe tena, mbona hatujawahi kupingana wala kushindwana hiyo
nitakulipa tu.
MAMA MBOKSINYO.
Siyo utanilipa ndo ulipe sasa. Kwanza unakula
nini maana supu ya miguu ya kuku ndo inaishia-ishia hivyo
RED.
Aaah! Bi mdashi embu nifanyie maajabu mapema
mambo yasije yakaharibika maana hapa nahisi kama vile tumbo linacheza singeli..
{Maneno ya Red yanawafanya watu wote
walioko mgahawani kucheka wakati huo mama mboksinyo anamtengea Red supu ya
miguu ya kuku}
MAMA MBOKSINYO.
Supu ya moto sana hii na ina pilipili ya
kutosha ngoja nikuletee na kijiko.
RED.
Kijiko chako cha nini wakati unajua kila siku
nakujaga ni kijiko changu.
MAMA MBOKSINYO.
Alafu wewe na nyatunyatu ndo mnaoongoza
kuniibia vijiko vyangu hapa mgahawani maana kila siku lazima vijiko viwili ama
vitatu vipotee.
RED.
Sinaga hizo pigo Bi mdashi, kwanza kijiko
changu nimekichora tatoo.
{Red anaingiza mkono mfukoni na kutoa
kijiko chake lakini kwa bahati mbaya mswaki aliouficha mfukoni nao unadondoka}
MAMA MBOKSINYO.
Jamani yaani haujawahi kuishiwa na maajabu
kabisa ona sasa unaficha hadi mswaki mfukoni. Alafu nikisema unaniibiaga vijiko
vyangu unaanza kuwaka.
Fade out.
GEREJI SINONI DARAJA MBILI (MCHANA)
EXT. SEBBY ANAPAMBANIA KOMBE.
{Sebby anahangaika kuziba pancha ya tairi
la lori huku jasho zito likimtoka, nayo njaa ikiwasha moto ndani ya tumbo lake}
SEBBY.
Dah! Ama kweli maandiko hayajawahi kudanganya
hata siku moja. Nimeamini wanaume tutakula kwa jasho.
{Baada ya njaa kali kumkabili sebby
anaamua kumkopa konki elfu moja walau akapate chochote kitu kwenye duka
lililopo pembezoni mwa gereji}
SEBBY.
Oya dingi naona hali ya tumbo haishikiki yaani
hapa nahisi njaa changanya na kiu alafu sina hata mia ya kusingiziwa hivyo
naomba uniazime buku nitakuvunjia badae tukishapatiwa vijisenti vyetu.
KONKI.
Poa chafu yao ila hakikisha unafanya kweli
hapo badae maana nadaiwa bili ya maji maskani yaani mambo si mambo.
SEBBY.
Poa mkali nitahakikisha.
{Sebby akiwa mwingi wa mawazo na mwenye
huzuni ya moyo anajifuta jasho na kusogea mpaka kwenye duka la mangi kununua juice
na skonsi}
SEBBY.
Yaani kila nilifanyalo
naona ni maseke tu. Madeni kila upande siyo kodi ya nyumba siyo chakula cha
asubuhi, mchana wala usiku.
{Sebby anafika
kwenye duka la mangi lakini anaweka mfukoni buku yake aliyopewa na konki na
kujaribu kumkopa mangi}
SEBBY.
Niaje broh! Mangi
MANGI.
Poa vipi chafu yao.
SEBBY.
Fresh tu kaka mkubwa.
MANGI.
Nipange mzee wa kazi
SEBBY.
Ebhanaee.. ndungu yangu hapa niko apeche
alolo alafu nina nenge hatari kama hautojali unikopeshe juisi ya jero na skonsi
kesho nitakuletea pesa yako
MANGI.
Poa ila ufanye kweli si
unajua hii ni biashara mzee.. alafu Juisi na skonsi mbona ni mbingu na ardhi
kwa kazi unayoifanya, si sawa na kumkabidhi kichaa rungu.
SEBBY.
Dah! Sasa nitafanyaje
kaka Mkubwa, wewe mwenyewe si unaona namna mazingira yalivyokaa kishingo upande.
MANGI.
Basi poa chafu yao.
SEBBY.
Shukrani kaka
{Sebby anabeba juisi
na skonsi yake kisha anarejea kibaruani lakini baada ya hatua tatu anapokea
ujumbe wa simu kutoka kwa mpenzi wake stella}
(Stella
sms)
“Hivi wewe mwanaume mbona
kama nakubembeleza sana yaani mpaka sasa haujanitumia pesa ya kusuka na shughuli
yenyewe imekaribia”
{Sebby anasikitika
na kitikisa kichwa chake kisha anaamua kurudisha majibu ya ujumbe wa stella}
(Sebby
sms)
“Jamani mpenzi wangu,
wewe mwenyewe unanijua kwamba sijawahi kuremba mwandiko nikiwa nacho ila ukiona
kimya ujue bado mambo hayajakaa sawa”
(Stella sms)
“Kwa hiyo unategemea mimi nifanyaje sasa”
(Sebby sms)
“Naomba nipe muda kidogo nishughulikie suala
lako tafadhali”
{Sebby anamjibu stella ilimradi
kumridhisha tu kwani mpaka wakati huo hakuwa na pesa nyingine zaidi ya buku
aliyoazimwa na stella}
SEBBY.
Ila huyu mwanamke atakuja kunipa presha bure
yaani laiti angelijua hali niliyo nayo kwa sasa asingelithubutu kuniomba hata
mia
{Sebby anajilaumu mwenyewe mara ghafla
apokea ujumbe mwingine wa simu kutoka kwa stella lakini anasita kuusoma na
kaamua kuizima simu yake}
Fade out.
NJIRO NYUMANI KWA KINA SABRINA (MCHANA)
INT. SABRINA ANASHINDWA KULA CHAKULA.
Kutokana na kugubikwa na mawazo yaliyojaa
hisia ndani yake sabrina anashindwa kula chakula cha mchana.
SABRINA.
Ila mapenzi upofu jamani yaani pamoja na
utajiri wote tulionao hapa kwetu ndo mimi huyu nimenasa hivi kwa huyu mwanaume.
{Sabrina anachukua simu yake na kumpigia
Sebby na wala asifanikiwe}
SABRINA.
Looh! Ndo ameamua
kunizimia na simu jamani
{Sabrina anajiegemeza kitandani mwake kwa
muda kidogo na baada ya dakika mbili simu yake inaita naye kwa bashasha anawahi
kuipokea akijua ni sebby kumbe hapana}
SABRINA.
Hovyoo.. yaani huyu naye sijui hata
nimwambiaje anielewe maana simtaki hata bure na kile kitambi chake.
{Sabrina anaamua kukata simu aliyopigiwa baada
ya kupata wazo la kufanya kwa wakati huo juu ya sebby}
SABRINA.
Pengine Sebby hana salio kwenye simu yake ndo
maana amenikaushia .
{Sabrina anaamua kuvuta kiasi cha laki
moja na nusu kwenye simu kutoka kwenye
akaunti yake ya benki na kumtumia sebby laki moja}
ITAENDELEA....
N.B- USISAHAU KUDONDOSHA COMMENT YAKO NI MUHIMU
PIA USIKOSE KUFUATILIA MIENDELEZO YA TAMTHILIYA MBALIMBALI KUTOKA KWA MTUNZI NA MWANDISHI SEBASTIAN S MASABHA
1.PESA ZA SHEMEJI
2. KONEKSHENI ZA VALENTINE
3. SUKARI YA KIJIJI
0 Comments